Posts

Showing posts from March, 2022

87. DENI YA DHAMBI ILIMALIZIKA

DENI YA DHAMBI ILIMALIZIKA 1.    Deni yangu ya dhambi, Yesu amelipa. Kwake msalabani Nilipewa uzima. Chorus: Deni ya dhambi, Msalabani, Ilimalizikia, Ni huru kabisa.   2.    Bwana Yesu asema, “Mwanangu dhaifu, Uwezo na ushindi Hupatikana kwangu.”   3.    Bwana, kweli naona, Nguvu zako pekee Huondoa ukoma, Niwe kipya kiumbe.   4.    Sina wema moyoni, Nidai neema, Nakubali kabisa, Kwa damu kusafiwa.   5.    Hata huko Mbinguni Miguuni pake, “Yesu alinifia,” Nitaimba milele.

88. NDIYO DAMU YA BARAKA

NDIYO DAMU YA BARAKA 1.    Ndiyo damu ya baraka ituoshayo wakosa, Kwake Bwana twaokoka, nasi twamsifu sasa; Nimestahili hukumu, siwezi kujitakasa; Nioshe katika damu, takuwa safi kabisa. Chorus: Safi kabisa; safi kabisa! Nioshe katika damu; Takuwa safi kabisa.   2.    Yesu alivikwa miiba, na kuangikwa Mtini, Na maumivu si haba yaliyompata chini. Nataka kijito hicho niende kuoga sasa; Ndicho kinitakasacho, nami ni safi kabisa.   Chorus: Safi kabisa; safi kabisa! Ndicho kinitakasacho, Nami ni safi kabisa.   3.    Baba, kweli nimekosa, moyo wangu ni dhaifu; Dhambi ni nyingi kabisa, nipate wapi wokovu? Yesu kijitoni pako, naja naamini sasa; Nioshe kwa damu yako, takuwa safi kabisa. Chorus:   Safi kabisa; safi kabisa! Nioshe kwa damu yako, Nami ni safi kabisa.

89. KWA KALVARI

KWA KALVARI 1.    Muda mwingi nilipotea, Sikufahamu msalaba, Wala aliyenifilia, Kwa Kalvari.   Chorus: Rehema bure na neema, Samaha nalo nilipewa, Ndipo aliponifungua, Kwa Kalvari.   2.    Kwa neno lake Bwana Mungu, Nilijiona mimi mwovu, Nikageuka na kutubu, Kwa Kalvari.   3.    Yote kwa Yesu namtolea, Ndiye mfalme wa pekee sasa, Kwa furaha nitamwimbia, Kwa Kalvari.   4.    Jinsi pendo lilivyo kuu, Neema ilishuswa toka juu, Alitufanyia wokovu, Kwa Kalvari.

90. ALITESWA, ALITESWA

ALITESWA, ALITESWA 1.    Aliteswa, aliteswa, Msalabani Yesu aliteswa, Dhambi zangu ameziondoa, Mahali pangu aliumizwa.   2.    Alikufa, alikufa, Msalabani Yesu alikufa, Kwa kifo chake nakombolewa, Kwa kuwa Yesu alinifia.   3.    Kafufuka, kafufuka, Kaburini Yesu alitoka, Nami nimewekwa huru pia, Kwa kuwa Yesu alifufuka.   4.    Yuko hai, yuko hai, Mbinguni anaishi Mwombezi, Daima huniombea mimi, Kwa kuwa Yesu adumu hai.   5.    Atarudi, atarudi, Siku moja Yesu atarudi, Na tutamwonapo tutafurahi, Kwa kupelekwa kwake Mbinguni.   6.    Sifa kwake, sifa kwake, Mbinguni na huimbwa milele, Kwa furaha, masifu, na shangwe, Tutamwimbia Yesu milele.

91. MAPENZI YAKO YAFANYIKE BWANA

MAPENZI YAKO YAFANYIKE BWANA 1.    Mapenzi yako yafanyike, Wewe mfinyanzi, nami towe, Unifinyange upendavyo, Mimi tayari, naja kwako.   2.    Mapenzi yako yafanyike, Unihojie dhambi zote, Unisafishe vya kimwili, Niinamapo Msalabani.   3.    Mapenzi yako yafanyike, Mimi dhaifu, mimi mnyonge. Uwezo wote, kwako kweli, Sasa niponye, Ee, Mwokozi.   4.    Mapenzi yako yafanyike, Natoa kwako vitu vyote, Maisha, mali, moyo, mwili, Vyote ni vyako, kweli, kweli.   5.    Mapenzi yako yafanyike, Mapenzi yangu yavunjike, Ninakubali uwe Bwana, Ni mali yako, twaa kabisa.   6.    Mapenzi yako yafanyike, Unitawale siku zote, Sura ya Yesu umba kwangu, Nijaze Roho nayo nguvu.

92. NATAKA NIMJUE YESU

NATAKA NIMJUE YESU 1.    Nataka nimjue Yesu, Na nizidi kumfahamu, Nijue pendo lake, na Wokovu wake kamili.   Chorus: Zaidi, zaidi, nimfahamu Yesu, Nijue pendo lake, na wokovu wake kamili.   2.    Nataka nione Yesu, Na nizidi kusikia, Anenapo kitabuni, Kujidhihirisha kwangu.   3.    Nataka nifahamu, na Nizidi kupambanua Mapenzi yake, nifanye Yale yanayompendeza.   4.    Nataka nikae naye, Kwa mazungumzo zaidi, Nizidi kuwaonyesha Wengine wokovu wake.

93. BWANA AMEFUFUKA

BWANA AMEFUFUKA 1.    Bwana amefufuka, Aleluya. Twimbe na malaika, Aleluya. Sifa zetu na shangwe, Aleluya. Na zao zisitengwe, Aleluya.   2.    Ukombozi timamu, Aleluya. Umetimu kwa damu, Aleluya. Mshindi asifiwe, Aleluya. Yu hai kwa milele. Aleluya.   3.    Jiwe, lindo, muhuri, Aleluya. Vi wapi? Na kaburi? Aleluya. Kifo hakimuweki, Aleluya. Ametoka peponi, Aleluya.   4.    Yu hai mtukufu; Aleluya. Cha kifo hatuhofu! Aleluya. Alitufia sisi, Aleluya. Tuwe mahuru nasi, Aleluya.   5.    Kichwa chatangulia, Aleluya. Tupae, nasi, pia!, Aleluya. Kwa kuwa tuna fungu, Aleluya. Mti, kaburi, mbinguni, Aleluya.   6.    diwe Mwokozi wetu, Aleluya. Sifa ni yako Yesu, Aleluya. Utukuzwe pekeo, Aleluya. Ni wewe ufufuo, Aleluya.

94. SIKU YA MBINGU KUJAWA NA SIFA

SIKU YA MBINGU KUJAWA NA SIFA 1.    Siku ya Mbingu kujawa na sifa, Dhambi zilizidi duniani; Yesu akaja azaliwe mtu, Awe na watu ulimwenguni.   Chorus: Alinipenda, alinifia, Ameondoa na dhambi zangu; Alikufa nipewe haki, Yuaja tena Mwokozi wangu.   2.    Na siku moja walikwenda naye, Wakamkaza msalabani; Aliumia, aliaibishwa, Ili atuokoe dhambini.   3.    Siku hiyo wakamlaza chini Kaburini alipumzika; Matumaini yetu wenye dhambi, Ni mwokozi, kwake twaokoka.   4.    Kaburi likashindwa kumshika; Jiwe likatoka mlangoni, Alifufuka kwa kushinda kwake, Naye yuko milele Mbinguni.   5.    Siku moja atatujia tena; Utukufu wake tutaona; Atawaleta na wapenzi wetu; Mwokozi wangu, tutaonana.

95. HIVI VITA VIMEKOMA

HIVI VITA VIMEKOMA   1.    Hivi vita vimekoma, Vimeshindwa na uzima, Na asifiwe daima, Bwana Yesu. Chorus: Aleluya! Aleluya! Aleluya!   2.    Nguvu za kifo ni hizo, Ila hazina uwezo, Ndizo sasa avunjazo, Bwana Yesu.   3.    Siku tatu za huzuni, Kisha atoka ufuni, Asifiwe duniani, Bwana Yesu.   4.    Mapingu ameyavunja, Mbingu amezifunga, Nasi sasa twamwimbia, Bwana Yesu.   5.    Na ulivyopigwa wewe, Ni kwamba tufunguliwe, Milele na usifiwe, Bwana Yesu.

96. MLE KABURINI, YESU MWOKOZI

MLE KABURINI, YESU MWOKOZI 1.    Mle kaburini, Yesu Mwokozi! Alilazwa chini, Bwana wangu! Chorus:   Bwana! Amefufuka, Kifo kimeshindwa kabisa! Gizani mle alitoka chini, Sasa atawala huko Mbinguni! Yu hai! Yu hai! Bwana Yesu yu hai!   2.    Aungoja huo, Yesu Mwokozi! Mchana ujao, Bwana wangu!   3.    Walinda kaburi, Yesu Mwokozi! Bure ni muhuri, Bwana wangu!   4.    Kifo kimeshindwa, Yesu mwokozi! Pingu zimevunjwa, Bwana wangu!

97. TAZAMENI HUYO NDIYE

TAZAMENI HUYO NDIYE 1.    Tazameni huyo ndiye, Mwenye kushinda vita; Haya, tumsujudie; Nyara anazileta; Watu wote msifuni, Sasa yumo kitini.   2.    Msifuni malaika, Mtukuzeni sana, Wote waliookoka Watamsifu Bwana; Watu wote msifuni, Sasa yumo kitini.   3.    Walimfanya dhihaka Zamani wenye shari, Kwao waliookoka Ni Bwana wa fahari; Watu wote msifuni, Sasa yumo Kitini.   4.    Nyimbo nzuri, sikizeni, Ni nyimbo za sifa kuu, Za Bwana Yesu kitini, Kutawazwa, yeye tu; Watu wote msifuni, Sasa yumo Kitini.

98. HUYO NDIYE! ANASHUKA

HUYO NDIYE! ANASHUKA 1.    Huyo ndiye! anashuka, Aliyetufilia, Wengi waliookoka, Wakimfurahia, Aleluya! Yesu aturudia.   2.    Sote tutamtazama, Amekaa kitini, Nao waliomchoma, Kumkaza mtini, Na kilio, wamuone enzini.   3.    Alama za kifo chake Hata sasa anazo Na waaminifu wake Wapendezewa nazo. Alipata, Kwetu alama hizo.   4.    Wokovu utakiwao Sasa wapatikana, Na watakatifu hao Mbinguni wakutana Kumlaki, Ndiyo siku ya Bwana   5.    Wakusujudie wote Mbele ya kiti chako. Zako, Bwana, nguvu zote Itwae miliki yako Njoo Bwana, Sisi tu watu wako.

99. MAELFU NA MAELFU

MAELFU NA MAELFU 1.    Maelfu na maelfu Wenye nguo bora! Masafu ya waongofu Wenye na bendera! Amekwisha kamili Vita vya shetani Fungueni lango hili; Njoni, ingieni!   2.    Imbeni aleluya, Zipae Mbinguni! Pigeni sana sauti Kwa kutumaini! Kwa hiyo viliumbwa Nchi hata Mbingu Dhiki za muda zikisha, Asifiwe Yesu.   3.    Loo! Tukionana Pwani ya ng’amboni! Loo! Tukishirikiana Milele Mbinguni! Midomo yote pia, Huko itaimba Wajane kufufukiwa Na kila yatima!   4.    Himiza enzi yako, Uliyetufia Utimize watu wako, Wakosaji pia, Mpendwa wa taifa Twakutumaini! Uzifunue ishara Urudi enzini!

100. TUMRUDIE BWANA

TUMRUDIE BWANA 1.    Mbona washangaa njiani? Mbona warejea nyuma? Warudi tena gizani Alimokutoa Bwana?   2.    Ni ya bure yote haya, Uliyofunzwa ya Mungu? Ni bure amekufia Bwana Yesu kwa uchungu?   3.    Wamtia kristo aibu Na maneno yake pia? Siku yaja ya hesabu, Utamjibuje Bwana?   4.    Upandapo tena hayo, Halafu utayavuna. Rudi kwa Bwana upesi, Mwombe akupokee tena.

101. TWONANE MILELE

TWONANE MILELE 1.   Nyimbo na tuziimbe tena Za alivyotupenda mbele; Kwa damu ya thamani sana! Mbinguni twonane milele. Chorus:   Twonane milele, Twonane bandarini kule; Twonane milele, Twonane bandarini kule.   2.   Hupozwa kila aoshwaye, Kwa damu ya Kondoo yule; Ataishi afurahiye Vya Yesu mbinguni milele.   3.   Hata sasa hufurahia Tamu yake mapenzi yale, Je, kwake tukifikilia, Kutofarakana milele?   4.   Twende mbele kwa jina lake, Hata aje mwokozi yule, Atatukaribisha kwake, Tutawale naye milele.   5.   Sauti zetu tuinue Kumsifu Mwokozi yule, Ili watu wote wajue Wokovu u kwake milele.

102. KAZI YANGU IKIISHA

KAZI YANGU IKIISHA   1.    Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka; Na kuvaa kutokuharibika, Nitamjua Mwokozi nifikapo ng’amboni; Atakuwa wa kwanza kunilaki.   Chorus: Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso; Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari.   2.    Furaha nitapata nikiona makao Bwana aliyotuandalia; Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo Vilivyonipa pahali Mbinguni.   3.    Nao waliokufa katika Bwana Yesu, Nitawaona tena huko juu; Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni, Nataka kumwona Mwokozi kwanza.   4.    Milangoni mwa mji Bwana atanipisha, Pasipo machozi wala huzuni. Nitauimba wimbo wa milele; lakini Nataka kumwona Mwokozi kwanza.

103. KAA NAMI

KAA NAMI 1.    Kaa nami, ni usiku tena; Usiniache gizani, Bwana; Msaada wako haukomi; Nili peke yangu, kaa nami.   2.    Siku zetu hazikawi kwisha, Sioni la kunifurahisha; Hakuna ambacho hakikomi, Usiye na mwisho kaa nami.   3.    Nina haja nawe kila saa; Sina mwingine wa kunifaa; Mimi nitaongozwa na nani Ila wewe Bwana, kaa nami.   4.    Sichi neno uwapo karibu; Nipatalo lote, si taabu; Kifo na kaburi haviumi; Nitashinda kwako, kaa nami.   5.    Nilalapo nikuone wewe, Gizani mote nimulikie; Nuru za mbinguni hazikomi, Siku zangu zote kaa nami.

104. TWASOMA NI NJEMA SANA

TWASOMA NI NJEMA SANA 1.    Twasoma, ni njema sana Mbinguni, kwa Bwana; Twasoma, dhambi hapana, Mbinguni kwa Bwana; Malaika wema wako, Vinanda vizuri viko, Na majumba tele yako, Mbinguni kwa Bwana.   2.    Siku zote ni mchana, Ni nchi ya raha; Wala machozi hapana, Ni nchi ya raha; Walioko wauona Uso wa Mwokozi, tena Jua jingine hapana, Ni nchi ya raha.   3.    Nyama na vitu viovu Havimo kabisa; Kifo nacho, na ubovu, Havimo kabisa. Ni watakatifu wote, Wameoshwa dhambi zote; Wasiosafiwa wote Hawamo kabisa.   4.    Tuna dhambi, pia sote, Mwokozi akafa; Kwake tutaoshwa zote, Mwokozi akafa; Kwake twapata wokovu, Tutawona utukufu; Mbinguni tutamsifu; Mwokozi akafa.   5.    Baba, mama, ndugu zetu, Twendeni kwa Bwana; Huku chini sio kwetu, Twendeni kwa Bwana; Tusishikwe na dunia, Na dhambi kutulemea; Tutupe vya chini pia, Twendeni kwa Bwana.

105. KUWATAFUTA WASIOWEZA

KUWATAFUTA WASIOWEZA 1.    Kuwatafuta wasioweza, Kuomba wamrejee Yesu, Kuwaambia maneno yake, “Njooni kwangu, nawapenda”.   Chorus: Nitakwenda, (kwenda), niwatafute Waongofu (wa Bwana) wageuke, Waingie (wote) katika zizi La Mkombozi (wetu) Yesu kristo.   2.    Kuwatafuta wasioweza, Waonyeshwe Mwokozi wetu, Kuwaongoza, wapate wote Uzima wa milele.   3.    Kazi hiyo nataka kufanya, Leo nimesikia mwito Kuwainua waangukao, Waletwe kwake Yesu njia.

106. MUNGU AWE NANYI DAIMA

MUNGU AWE NANYI DAIMA 1.    Mungu awe nanyi daima, Hata twonane ya pili, Awachunge kwa fadhili, Mungu awe nanyi daima. Chorus: Hata twonane huko juu, Hata twonane kwake kwema; Hata twonane huko juu, Mungu awe nanyi daima.   2.    Mungu awe nanyi daima; Ziwafunike mbawaze, Awalishe, awakuze; Mungu awe nanyi daima.   3.    Mungu awe nanyi daima; Kila wakati wa shani Awalinde hifadhini; Mungu awe nanyi daima.   4.    Mungu awe nanyi daima; Awabarikie sana, Awapasulie kina; Mungu awe nanyi daima.

107. EWE, BABA WA MBINGUNI

EWE, BABA WA MBINGUNI   1.    Ewe, Baba wa Mbinguni, Usikie twombalo Hapa chini duniani, Na uwe radhi nalo.   Chorus: Ee Mungu, bariki Ndugu hawa wawili! Ee Mungu, bariki Ndugu hawa wawili!   2.    Watu hawa mbele zako, Na mbele ya kanisa; Watimize Neno lako Wanakutana sasa.   3.    Kama Yesu na Kanisa, Ni mmoja, na hivyo, Watu hawa wape sasa Wawe mmoja vivyo.   4.    Walinde, Bwana, daima, Wabariki nyumbani Uwape nyingi salama Humu ulimwenguni.   5.    Wabariki, ewe Bwana, Watu hawa wawili, Wape upaji wa wana, Wafurahishwe kweli.   6.    Siku zao duniani Zitakapopungua, Wape kurithi Mbinguni Mema ya kwendelea.

108. TWENENDE SAYUNI

TWENENDE SAYUNI 1.    Mpendao Bwana Ije raha yenu! Imbeni nyimbo za raha Wa ibada yenu. Chorus:   Twenende Sayuni, Mji mzuri Sayuni; Twenende juu Sayuni Ni maskani ya Mungu.   2.    Wasiimbe wao Wasioamini, Watoto wa Mungu ndio Waimbao chini.   3.    Twaona rohoni Baraka za Mungu, Tusijafika Mbinguni Kwenye utukufu.   4.    Tutakapo mwona Masumbuko basi, Huwa maji ya uzima, Anasa halisi.   5.    Tupaaze sauti, Na fute machozi, Twenenda kwa Imanweli Naye ni Mwokozi.

109. NITAIMBA YA YESU

NITAIMBA YA YESU 1.    Nitaimba ya Yesu, Kwa rehema zake, Baraka nyingi sana Nimepata kwake; Nitaimba ya Yesu, Sadaka ya Mungu, Alimwaga damu Ukombozi wangu.   2.    Nitaimba ya Yesu Hapa siku zote, Nitakapokumbuka Vyema vyake vyote; Nitaimba ya Yesu Hata mashakani, Yeye atanilinda Mwake ubavuni.   3.    Nitaimba ya Yesu Niwapo Njiani; Takaza mwendo, hata Nifike Mbinguni; Nikiisha ingia Mlangoni mle, Yesu nitamwimbia Mbinguni milele.

110. MAPYA NI MAPENZI HAYO

MAPYA NI MAPENZI HAYO 1.    Mapya ni mapenzi hayo, Asubuhi tuonayo, Saa za giza hulindwa Kwa uzima kuamshwa.   2.    Kila siku, mapya pia Rehema, wema, na afya, Wokovu, na msamaha, Mawazo mema, furaha.   3.    Tukijitahidi leo Na mwendo utupasao, Mungu atatueleza Yatakayompendeza.   4.    Mambo yetu ya dunia Mungu atayang’aria, Matata atageuza Yawe kwetu ya baraka.   5.    Yaliyo madogo, haya Mungu tukimfanyia, Yatosha: tutafaidi Huvuta kwake zaidi.   6.    Ewe Bwana, siku zote, Tusaidie kwa yote: Mwendo wetu wote vivyo, Uwe kama tuombavyo.

111. NENO LAKO BWANA

NENO LAKO BWANA   1.    Neno lako, Bwana, Ni imara sana; Lilo latwongoza, Lilo latufunza.   2.    Adui wabaya Wakikaribia, Neno lake Bwana Ni ulinzi sana.   3.    Siku za dhoruba Soma ukiomba; Neno lake Bwana Msaada sana.   4.    Ukiliamini, Hwenda na amani; Una na furaha Neno ni silaha.   5.    Ni furaha kweli, Na wingi wa mali, Neno lake Bwana Kwa wasiokana.   6.    Neno la rehema, Tukali wazima; Faraja I papo, Tufarikanapo.   7.    Tulijue sana, Neno lako, Bwana, Hapa tukupende, Kisha kwako twende.